Sunday, 22 April 2012

Michango ya HOJA


CCM waenda mikoani kuukana ufisadi

*Wapeleka ujumbe wa NEC mkoa kwa mkoa
*Nape asema watapambana hadi washinde

Na Edmund Mihale, Dodoma

CHAMA Cha Mpinduzi (CCM) kimeanza ziara mikoani kupeleka ujumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM kwa wanachama kuwa kimedhamiria kupambana na ufisadi ndani na nje ya chama hadi kishinde.

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye aliyasema hayo Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma jana, wakati akitangaza ratiba ya mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Wilson Mukama na Sekretarieti ya chama hicho mkoani hapa.

Alisema chama hicho kimeandaa ziara kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa Halmashauri Kuu kwa wanachama wake kuanzia leo ambapo watafanya makutano katika Uwanja wa Nyerere Square na kesho Mkoani Morogoro.

Alisema kuwa mapokezi hayo yataendelea katika Mkoa wa Pwani Wilaya ya Kibaha ambapo yatapokelewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete. Alisema kuwa siku hiyo hiyo yataendelea katika Mkoa Dar es Salaam na Aprili 17 mwaka huu yatakuwa Zanzibar.

"Tutapambana na ufisadi hadi tushinde," alisema Bw. Nnauye.

Alisema kuwa CCM haitavumilia kuona inachafuliwa na watu wachache na kuwataka wanachama waliohama kwa hasira kutokana na kashfa ya ufisadi kurudi kundini.

Alisema uamuzi uliofikiwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa utafanyiwa kazi.Alisema uamuzi wa kuwachukulia hatua wanaojihusisha na ufisadi uko pale pale, hivyo wasidhani kuwa chama kimeishia hapo. 

"Ndugu zangu Halmashauri Kuu iliamua kuwa tutapambana na ufisadi hadi tushinde, hivyo kama alivyozungumza mwenyekiti, wanaotuhumiwa wajiandae, tumefunga milango na madirisha yote, ili kuhakikisha tunashinda," alisema Bw. Nnauye.

 Maoni:

   Nape hiyo sio njia ya kuushinda ufisadi. ccm itashinda tu ufisadi ikiwaweka ndani mafisadi wote na kutaifisha mali zote walizofisadi

  • nyie mnaosema mpo mjini ndio maana shudia maandamano ya ccm ndio utajua kuwa wanapendwa na wananguvu kubwa kaeni pembeni nendene mboe club mkaombe kazi mtapewa tu
  • Ni ngumu CCM kushinda ufisadi kwani mwenyekiti haamini kama upo. Itakuwaje amnyanyue mkono Lowasa mbele ya watanzania kuwa ndiye mgombea anayefaa Monduli? Hata kama maakama hajasibitisha lakini ripoti ya mwakyembe si ameisoma na Lowasa alipewa nafasi hakukana mbele ya bunge.Ufisadi ni best fiend wa CCM huwezi kuwatenganisha.Dawa si kuzunguruka mikoani, bali kushughulikia vilivyo mafisadi watuhumiwa wote. CCM hamjashtuka tu!kuwa watanzania wanaelimika kwa kasi kuhusu siasa!
  • HAWAWEZI KUSHUGHULIKIA MAFSADI KWA KUZUNGUKA NCHI NZIMA. KWANI HIYO SI DHAMIRA YAO, NI HADI VYAMA VYA UPINZANI NA WANANCHI WAPIGE KELELE WE, NDO WAJUE KUWA KUNA MAFISADI NDANI YA CHAMA. NI MIAKA MINGAPI SASA KELELE HIZO ZIMEPIGWA. UNAONA WANAVYOKURUPUKA HATA JINSI YA KUPAMBANA NA UFISADI NDANI YA CHAMA, ETI KUZUNGUKA NCHI NZIMA KUWAELEZA WANANCHI. HEBU WAFUKUZENI KABISA UANACHAMA TUONE KAMA MNA NIA YA DHATI KWELI YA KUPINGA UFISADI.

  • nakuaminiya Nnauye ccm chama makini na ishallah mungu akipenda kitaendelea kushinda tu siku hadi siku hawa chadema chama cha kibaguzi tushakiishutukizia kazi yao kueneza chuki tu ila kwa uwezo wa mola tutashinda tu ubunge ,udiwani,Uraisi na katika chaguzi zote za kisiasa hawa ambao wanapiga kelele ni wehu tu na wahuni ila ccm chama makini na kitaendelea kutawala mpaka kiama hapa hatutoi nchi mtazunguruka nchi nzima mpaka mtoke majasho ya ulimi lakini ccm itashinda tu na itaendelea kutawala daimaWewe unayesema hamtoi nchi 


    unamaana gani? ni ya mjomba wako kwani? unadhani Bhagbo alipenda kuiachia hata nyie tutawalazimisha kama mkikiuka utaratibu.
    NAPE HUWEZII! UMEWEKWA HAPO CHAMBO TU.Wewe na wenzio mnao ubavu wa kuumaliza ufisadi?Jitahidi lakini chunga sana usije poteza moto.wenye pesa huwawezi.Ndio maana wazee wamekutanguliza wewe!
  • Nape atanusa kama paka likimshinda anajeza nduki. Yetu macho kama wenye damu ya CCM WAMESHINDWA SEMBUSE SISIMIZI.

    CCM haiwezi kumtoa Lowassa, Chenge na Rostam kwenye chama, kama hawaitakii mema CCM basi wajaribu waone! Msitudanganye kuwa mmejivua GAMBA hii ni kukimbia kivuli chako! Iweje Mafisadi wapewe Siku 90 za kupima waone kama wanafaa kuendelea au? Huu ni uhuni na uonevu mkubwa hasa viongozi wa chini maana wao wakifanya makosa kidogo tu,atakimbizwa kama kuku kwenye nafaka! Kama kweli mwenyekiti alikuwa na nia ya kuwaondoa kwenye uongozi hao watu ni siku ile ile angewambia wajiuzulu! Mbona secretariete haikupewa muda wa kupima wao wamepewa? Huu ni uonecu na inathibitisha kuwa chama chetu ni cha watu wachache tena wafanyabiashara wakubwa na sio wakulima na wafanyakazi kama ilivyo kuwa hapo mwanzo! Kama tunataka kupata imani kwa wananchi kuvunja secretariet pekee hakutoshi! Waondoke wale wote wasiokitakia mema chama na wamekifanya kikose dira kwa vijana walio wengi! (maana wazee (Makada) waliowengi wanazidi kupungua kila kukicha)!
  • Kingine kinachofanya chama kikose Mvuto kwa jamii ni kule kuendekeza ufamilia katika chama, eti kisa ni mtoto wa fulani basi apewe nafasi (Mfano Ridhiwan, Nnape, Makamba, mwinyi, Karume, na wengine) Najua wengine mtarukia hoja kuwa kama wanasifa wasipewe? Lah hasha! Wapewe kwa kufuata utaratibu kama wengine wanavyofuata sio kwa kutoa favor (Kwa kuwa baba au mama ake ni fulani...). Tukumbuke yanayotokea Misri Libya na kwingine yalianza hivi hivi na mwishoe tukaona viongozi wakitaka kuwasimika watoto wao nyadhifa fulani kama hali hii haita dhibitiwa katika chama basi tutegemee yaliyotokea Misri.

    jamani nasema tena CCM ni chama makini chama cha wasomi sio chama cha kihuni au cha kikabila kama chadema ccm ni chama cha watu ambao walokwenda shule sio chama cha kichaga au cha kihaya hichi sisi msimamo wetu ni maendeleo kwa wananchi na hatutosita kuleta maendeleo kwa kelele zenu mwenye macho hambiwi tazama nchi toka alipoondoka nyerere maendeleo mangapi yamepatikana mpaka sasa acheni kelele zenu hizo nyinyi chadema ni watu hatari kama sumu ni wabinafsi na niwatu wajanja ambao mnataka nchi ili muweze kuitumia kwa masilahi yenu nakwambieni kama mmechelewa sio leo tena CCM sio daladala kila moja akawachiwa abande tu leo aje huyu kesho huyu serekali hatutoi ngo
  • Rostam na Lowassa walishiriki kwa kiasi kikubwa sana kumweka Kikwete madarakani mwaka 2005. Haiwezekani akawatupa. Hii ni danganya toto. Haiwezekani Lowasa aliilazimisha Tanesco kuingia mkataba na Richmond/Dowans (ambayo Rostam ni mbia)bila Kikwete kujua.Mali ya kifisadi ya akina Rostam ilisaidia kumwingiza Kikwete ikulu; kwa hiyo atawatupa hadharani tu lakini ndani lazima awasidie. Kumbuka Kikwete alipochukua uenyekiti tu, alimfanya Rostam kuwa mweka hazina wa ccm.
  • CCM ni chama cha siasa. chama cha siasa kinawezaje kumpeleka mtuhumiwa mahakamani? hiyo ni kazi ya dola,,walaumiwe serikali na watu wake, maana hata watu wa Chadema wamo serikalini ndo mna wanaweza kusema uwongo na wasichukuliwe hatua.
  •            the GREEN planetApr 22, 2012 05:48 AM
  • Hii ndio CCM naamini ni Chama Cha Siasa na Si Chama Cha SI HASA.wanajua wanacho kifanya.Wanauzoefu wa kushughulikia WAKENGEUFU wa Malengo na IMANI ya chama chao ambao kwa sasa tunawaita MAFISADI. wakati wa chama kimoja walikuwepo pia lakini walishughulikiwa kwa OPERATION maalum kama Azimio La Arusha, Uhujumu wa Uchumi, Fagio la Chuma nk kwa kizazi kile.

    Kwa kizazi hiki cha watu waliojaa ujanjaujanja naamini wanawashughulikia kwa MTINDO maalum. Wakikurupuka tu,hao hao wanaoitwa MAFISADI watahamia kwao na kwa kuwa wamejaaliwa kuupepeta watawasafisha na kwa hakika watakuwa safi wao na mihela yao.

    Imani yangu kuwa MTINDO wa CCM wanaoutumia uko sahihi DELAYING TACTICS ili HAO,WEWE NA MIMI tuwasemeeeeeeeeee Tuwachafuweeeeee Tuwaumbueeeeee na kama ushahidi upo tuendelee kuwaanikaaaaaaaaaa
    wasifae kabisa kabisa si kwa CCM na Kwa WAO hapo lengo la CCM linakamilika bila KUIATHIRI. Halafu sasa mdogomdogo haooooooooooooooooooo

    Mambo ya Shule sio KUKOPI NA KUPESTI baba kuwa mpole HII NDO CCM

No comments:

Post a Comment