HOJA YA ZITTO YA KUTAKA WAZIRI MKUU PINDA, APIGIWE KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NAYE YAKOSA SAPOTI YA KANUNI ZA BUNGE

Spika Anna Makinda
NA MWANDISHI WETU, DOM
Spika wa Bunge, Anne Makinda amesema hoja ya kutaka kumpigia kura ya kutokuwa na imani Waziri Mkuu Mizengo Pinda, inayokusudiwa kupelekwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini ,Zitto Kabwe (Chadema), ni batili na haina nguvu kwa kuwa haijakidhi matakwa ya kanuni.
Amewataka wabunge kuzisoma kikamilifu kanunzi zinazohusiana na hoja hiyo.
Wakati Spika Anna akieleza hivyo, wabunge nao wamesema wana imani na utendaji kazi wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na wasingepanda kumwondoa katika wadhifa huo, lakini tatizo kubwa ni mawaziri wake.
Pia, wamesema hoja ya kutaka kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye, inalenga kumshinikiza kuwawajibisha mawaziri wanaotuhumiwa kwa vitendo vya wizi na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Wakijadili taarifa za Kamati za Hesabu za Mashirika ya Umma, Serikali za Mitaa na Serikali Kuu, wabunge waliwashutumu mawaziri kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kiasi cha wengine kwenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu kuwa mawaziri wengi ni wezi na kwamba, wamekuwa wakijali maslahi binafsi kuliko ya wananchi wanaowaongoza.
Mawaziri waliokuwa wakishutumiwa na kutakiwa kuachia ngazi ni Mustafa Mkullo (Fedha), Dk. Cyril Chami (Viwanda na Biashara), George Mkuchika (TAMISEMI), Omar Nundu (Uchukuzi), ambapo wabunge waliwataka kuachia ngazi.
Kutokana na tuhuma hizo, Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini-CHADEMA), alitoa pendekezo la kuwataka wabunge 70 kusaini ili kuwasilisha hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu.
Habari zilizopatikana bungeni jana zimesema wabunge 62 kati 70 wanaotakiwa, wamesaini pendekezo hilo huku wanne wakitoka CCM na mbunge pekee wa UDP, John Cheyo ndiyo hajasaini.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana, Zitto na Deo Filikunjombe (Ludewa-CCM), ambao ndiyo wanaratibu shughuli hiyo, walisema tatizo kubwa la wabunge si Waziri Mkuu Pinda bali mawaziri wasio waaminifu.
Zitto alisema tayari kazi ya kukusanya saini inaendelea na wana imani hadi kufikia leo jioni wangekuwa wamekamilisha idadi ya 70 kama kanuni inavyosema.
Amesema wabunge wa vyama vyote wamesaini ispokuwa UDP na kwamba, uongozi wa CUF umetoa maelekezo maalumu kwa wabunge wake kusaini.
Alisema miongoni mwa wabunge waliosaini wanne wanatoka CCM na kwamba, hoja hiyo ni ya wabunge wote bila kujali itikadi za vyama na lengo ni kutengeneza Bunge la utendaji badala ya kulalamika.
Iwapo hoja hiyo itapitishwa na Bunge, Pinda atakuwa Waziri Mkuu wa kwanza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye.
Zitto amesema kuwa wanatarajia kuwasilisha hoja hiyo kwa Spika wa Bunge, Jumatatu kwa ajili ya hatua zaidi
CHADEMA WAFUKUZANA KIGOMA
CHADEMA wametangaza kumfukuza uanachama Mwenyekiti wa jimbo la Kigoma Kusini, Jumanne Bilango kwa tuhuma za kukiuka maadili ya uongozi.
Hatua hiyo imetangazwa na Katibu wa chama hicho jimboni humo, Shaban Madede, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye soko la Kazuramimba na kueleza kuwakamati ya sektretarieti ya jimbo imeridhia uamuzi uliochukuliwa na tawi la CHADEMA la Kazuramimba kumvua uanachama Mwenyekiti huyo.
Madede alisema tuhuma kubwa dhidi ya Mwenyekiti huyo inaelezwa kuwa alishindwa kuwasilisha sh. 250,000 zilizotolewa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe mwaka 2004 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari ya kata hiyo.
CHADEMA WACHEMSHA NA DANGANYA TOTO
Wabunge wa CHADEMA ambao awali walitangaza kususia uchaguzi huo, walishiriki ikiwa ni pamoja na kusimamisha mgombea wake Anton Komu, ambaye alibwagwa vibaya.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bunge, Freeman Mbowe, alisema hawatashiriki uchaguzi kwa madai ya kutokuwa huru na haki.
Mbowe, ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, alisema wabunge wa chama hicho watatoka nje na hawatakuwa tayari kuwasikiliza wagombea wala kupiga kura na kwamba CHADEMA kushiriki uchaguzi huo ni kutowatendea haki Watanzania, lakini katika hali ya kushangaza wabunge hao wakiongozwa na Mbowe walishiriki uchaguzi huo na hawakutoka ukumbini.
Awali, CHADEMA lilitaka kupewa nafasi moja kwa ajili ya chama hicho pekee badala ya kushindaniwa na wapinzani wote kama kanuni inavyoelekeza.
‘Sisi kama Chadema hatutashiriki katika uchaguzi huo wala hatutashiriki kupiga kura wala kusikiliza tutatoka nje tuache waendelee,’ alisema.
Hata hivyo, Naibu Spika Job Ndugai, alisema hoja hiyo ya CHADEMA haina msingi na kwamba, nafasi mbili walizopewa wapinzani zitahusisha vyama vyote vya upinzani.
Awali, wagombea waliingia katika nafasi hiyo ni Bernard Murunya, Adam Kimbisa, Makongoro Nyerere, Mrisho Gambo, Siraju Kaboyonga, William Malecela, Dk. Evans Rweikiza, Elibariki Kingu na Dk. Edmund Mndolwa wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). Pia, yumo John Lifa-Chipaka wa TADEA.
Kwa upande wa wanawake mchuano kuwania nafasi hiyo ulikuwa kwa Engela Kizigha, Fancy Nkuhi, Dk. Godbertha Kinyondo, Janet Mmari, Janeth Mbene, Mariam Ussi Yahya na Sebtuu Mohamed Nassor, Shyrose Bhanji, Sofia Ali Rijaal wote kutoka CCM wakati mgombea kutoka upinzani ni Rose Mwalusamba (CUF).
Waliowania nafasi ya kuwakilisha Zanzibar katika Bunge la Afrika Mashariki walikuwa ni Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Dk. Ahmada Hamad Khatib, Dk. Haji Mwita Haji, Khamis Jabir Makame, Dk. Said Gharib Bilal na Zubeir Ali Maulid wote kutoka CCM.
Kwa upande wa wagombea wa vyama vya upinzani, walikuwemo Dk. Fortunatus Masha (UDP), Anthony Komu (CHADEMA), Juju Danda (NCCR-MAGEUZI), Micah Mrindoko (TLP), Mwaiseje Polisya (NCCR-MAGEUZI), Nderakindo Kessy na Twaha Issa Taslima (CUF).
HOJA YA ZITTO YA KUTAKA WAZIRI MKUU PINDA, APIGIWE KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NAYE YAKOSA SAPOTI YA KANUNI ZA BUNGE
![]() |
| Spika Anna Makinda |
NA MWANDISHI WETU, DOM
Spika wa Bunge, Anne Makinda amesema hoja ya kutaka kumpigia kura ya kutokuwa na imani Waziri Mkuu Mizengo Pinda, inayokusudiwa kupelekwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini ,Zitto Kabwe (Chadema), ni batili na haina nguvu kwa kuwa haijakidhi matakwa ya kanuni.
Amewataka wabunge kuzisoma kikamilifu kanunzi zinazohusiana na hoja hiyo.
Wakati Spika Anna akieleza hivyo, wabunge nao wamesema wana imani na utendaji kazi wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na wasingepanda kumwondoa katika wadhifa huo, lakini tatizo kubwa ni mawaziri wake.
Pia, wamesema hoja ya kutaka kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye, inalenga kumshinikiza kuwawajibisha mawaziri wanaotuhumiwa kwa vitendo vya wizi na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Wakijadili taarifa za Kamati za Hesabu za Mashirika ya Umma, Serikali za Mitaa na Serikali Kuu, wabunge waliwashutumu mawaziri kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kiasi cha wengine kwenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu kuwa mawaziri wengi ni wezi na kwamba, wamekuwa wakijali maslahi binafsi kuliko ya wananchi wanaowaongoza.
Mawaziri waliokuwa wakishutumiwa na kutakiwa kuachia ngazi ni Mustafa Mkullo (Fedha), Dk. Cyril Chami (Viwanda na Biashara), George Mkuchika (TAMISEMI), Omar Nundu (Uchukuzi), ambapo wabunge waliwataka kuachia ngazi.
Kutokana na tuhuma hizo, Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini-CHADEMA), alitoa pendekezo la kuwataka wabunge 70 kusaini ili kuwasilisha hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu.
Habari zilizopatikana bungeni jana zimesema wabunge 62 kati 70 wanaotakiwa, wamesaini pendekezo hilo huku wanne wakitoka CCM na mbunge pekee wa UDP, John Cheyo ndiyo hajasaini.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana, Zitto na Deo Filikunjombe (Ludewa-CCM), ambao ndiyo wanaratibu shughuli hiyo, walisema tatizo kubwa la wabunge si Waziri Mkuu Pinda bali mawaziri wasio waaminifu.
Zitto alisema tayari kazi ya kukusanya saini inaendelea na wana imani hadi kufikia leo jioni wangekuwa wamekamilisha idadi ya 70 kama kanuni inavyosema.
Amesema wabunge wa vyama vyote wamesaini ispokuwa UDP na kwamba, uongozi wa CUF umetoa maelekezo maalumu kwa wabunge wake kusaini.
Alisema miongoni mwa wabunge waliosaini wanne wanatoka CCM na kwamba, hoja hiyo ni ya wabunge wote bila kujali itikadi za vyama na lengo ni kutengeneza Bunge la utendaji badala ya kulalamika.
Iwapo hoja hiyo itapitishwa na Bunge, Pinda atakuwa Waziri Mkuu wa kwanza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye.
Zitto amesema kuwa wanatarajia kuwasilisha hoja hiyo kwa Spika wa Bunge, Jumatatu kwa ajili ya hatua zaidi
CHADEMA WAFUKUZANA KIGOMA
Hatua hiyo imetangazwa na Katibu wa chama hicho jimboni humo, Shaban Madede, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye soko la Kazuramimba na kueleza kuwakamati ya sektretarieti ya jimbo imeridhia uamuzi uliochukuliwa na tawi la CHADEMA la Kazuramimba kumvua uanachama Mwenyekiti huyo.
Madede alisema tuhuma kubwa dhidi ya Mwenyekiti huyo inaelezwa kuwa alishindwa kuwasilisha sh. 250,000 zilizotolewa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe mwaka 2004 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari ya kata hiyo.
CHADEMA WACHEMSHA NA DANGANYA TOTO
Wabunge wa CHADEMA ambao awali walitangaza kususia uchaguzi huo, walishiriki ikiwa ni pamoja na kusimamisha mgombea wake Anton Komu, ambaye alibwagwa vibaya.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bunge, Freeman Mbowe, alisema hawatashiriki uchaguzi kwa madai ya kutokuwa huru na haki.
Mbowe, ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, alisema wabunge wa chama hicho watatoka nje na hawatakuwa tayari kuwasikiliza wagombea wala kupiga kura na kwamba CHADEMA kushiriki uchaguzi huo ni kutowatendea haki Watanzania, lakini katika hali ya kushangaza wabunge hao wakiongozwa na Mbowe walishiriki uchaguzi huo na hawakutoka ukumbini.
Awali, CHADEMA lilitaka kupewa nafasi moja kwa ajili ya chama hicho pekee badala ya kushindaniwa na wapinzani wote kama kanuni inavyoelekeza.
‘Sisi kama Chadema hatutashiriki katika uchaguzi huo wala hatutashiriki kupiga kura wala kusikiliza tutatoka nje tuache waendelee,’ alisema.
Hata hivyo, Naibu Spika Job Ndugai, alisema hoja hiyo ya CHADEMA haina msingi na kwamba, nafasi mbili walizopewa wapinzani zitahusisha vyama vyote vya upinzani.
Awali, wagombea waliingia katika nafasi hiyo ni Bernard Murunya, Adam Kimbisa, Makongoro Nyerere, Mrisho Gambo, Siraju Kaboyonga, William Malecela, Dk. Evans Rweikiza, Elibariki Kingu na Dk. Edmund Mndolwa wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). Pia, yumo John Lifa-Chipaka wa TADEA.
Kwa upande wa wanawake mchuano kuwania nafasi hiyo ulikuwa kwa Engela Kizigha, Fancy Nkuhi, Dk. Godbertha Kinyondo, Janet Mmari, Janeth Mbene, Mariam Ussi Yahya na Sebtuu Mohamed Nassor, Shyrose Bhanji, Sofia Ali Rijaal wote kutoka CCM wakati mgombea kutoka upinzani ni Rose Mwalusamba (CUF).
Waliowania nafasi ya kuwakilisha Zanzibar katika Bunge la Afrika Mashariki walikuwa ni Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Dk. Ahmada Hamad Khatib, Dk. Haji Mwita Haji, Khamis Jabir Makame, Dk. Said Gharib Bilal na Zubeir Ali Maulid wote kutoka CCM.
Kwa upande wa wagombea wa vyama vya upinzani, walikuwemo Dk. Fortunatus Masha (UDP), Anthony Komu (CHADEMA), Juju Danda (NCCR-MAGEUZI), Micah Mrindoko (TLP), Mwaiseje Polisya (NCCR-MAGEUZI), Nderakindo Kessy na Twaha Issa Taslima (CUF).
MILLYA ADAIWA KUSEPA NA FEDHA ZA KUANZISHIA SACCOS YA UVCCM ARUSHA
![]() |
| James Ole Millya |
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa Arusha James Ole Millya ambaye ameshajipeleka Chadema amedaiwa kusepa na sh. milioni 2 alizokabidhiwa kwa ajili ya kuanzisha SACCOS ya UVCCM mkoani humo.
Habari zinasema, bunda hilo la sh. milioni 2 zilitolewa na Felix Mrema aliyekua mbunge wa Arusha mjini na Elisa Mollel aliyekua mbunge wa Arumeru Magharibi, walitoa hundi ya Sh.milioni 1 kila mmoja, Desemba 2008, katika Baraza la kwanza la Vijana lililofanyika Karatu.
Akizungumza na mtandao huu, Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM mkoani Arusha, Mrisho Gambo amemtaka Millya kurudisha fedha hizo haraka ili ziendeleze shughuli ya kuanzisha SACCOS mkoani hapa, kwa lengo la kujenga uchumi wa Vijana.
Aidha ametoa angalizo kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kumwangalia Millya ambaye ni mroho wa madaraka na mchochezi wa vurugu na kuwa,hata kama anataka kumudu mabadiliko ndani ya chama kipya, wampe nafasi moja tu Wilayani Monduli, waone kama atafanya kazi au majungu.
Gambo alisema kwanza wamefurahi Millya kuhamia Chadema,kwani alikuwa ni mtu anayesababisha pancha kwenye tairi,lenye gari kubwa na tangu Millya alipochaguliwa kuwa mwenyekiti hakuwahi kufanya Maendeleo yoyote ndani ya UVCCM,wala kuleta tija, bali alikuwa ni kiongozi mwenye kuleta migogoro na maandamano, kila kukicha ndani ya chama pamoja na kutetea mafisadi.
Alisema Millya anasumbuliwa na uroho wa madaraka akitoa mfano alitaja mwaka 2010 aligombea nafasi na Mbunge wa Simanjiro,Christopher Ole Sendeka,akashindwa na umri wake pia umepita kugombea tena nafasi ya UVCCM, ndio maana akaona bora akijiengue, kwani hana nafasi tena ya kugombea ndani ya CCM na kwakuwa alikosa nafasi ya kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki,akaona hapa ni pagumu na kuhamia Chadema.
Millya ameamua kufanya siasa ili apate kipato kwasababu ni kibaraka wa mafisadi na kuongoza msafara wa magamba dagaa, huku magamba makubwa yakijiandaa kuondoka.
“Tunamtaka atukabidhi ofisi na kulipa deni letu la Sh.milioni 2 zilizotolewa kwa ajili ya kuanzisha SACCOS na ameingiza hasara chama zaidi ya milioni 600,hivyo tunasema Millya ni msumari uliokuwa ukisababisha pancha, kila mara na kila wakijitahidi kuliondoa gari hilo,lilikuwa linawekwa kiraka na mafisadi, hivyo ni bora aliyekuwa akisababisha pancha kaondoka mwenyewe,”alisema.
Alisema kuwa kuhusu kauli kuwa amekosa nafasi ya Ubunge Afrika Mashariki na kumweka Gambo ambaye hana sifa kama zake,alisema kuwa sio kweli kwa sababu wote walikuwa na onyo ndani ya chama na wana digrii mbili, ila tofauti zao ni sifa ambazo yeye ni Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana Afrika Mashariki na Mchambuzi wa Mifumo ya Kompyuta Manispaa ya Arusha, tofauti na Millya hajulikani kazi yake wala anapoishi.


No comments:
Post a Comment